Kama
ulidhani ukimya wa Extra Bongo ni kifo cha bendi basi andika maumivu,
bendi inakuja kivingine kabisa ambapo mwishoni mwa wiki hii inaingia
kambini ikiwa na wasanii mchanganyiko wapya na wa zamani.
Mkurugenzi
wa bendi hiyo, Ally Chocky ameiambia Wataanashati wa Mujini kuwa bendi yake ilisitisha
maonyesho baada ya kufiwa na mkewe (Mama Shuu) ambaye nae mkurugenzi wa bendi hiyo.
“Tunaingia
kambini wiki ijayo (wiki hii), kambi ambayo haitazidi wiki mbili ikiwa
ni maalum kwaajili ya wanamuziki kutambuana na kushikana pamoja na
kutengeneza japo nyimbo chache mpya,” alisema Chocky na kuongeza kuwa
wataanza rasmi maonyesho yao mwezi Disemba.
“Tuna
wasanii wapya kutoka nje ya nchi na wachache wa hapa nyumbani,
tumesajili kwa kuzingatia mahitaji ya bendi, hatujakurupuka. Lengo letu
ni kuwa na kikosi kidogo lakini cha watu wachapakazi,” alifafanua Ally
Chocky.
No comments:
Post a Comment